Dkt. R.M. Wafula, alizaliwa katika kijiji cha Khalumuli ambacho hivi sasa kimo katika Sehemu ya Uwakilishi Bungeni ya Webuye. Miaka michache baadaye, wazazi wake walihamia Mbakalo, GArafa ya Tongaren. Alisomea katika Shule ya Msingi ya Mbakalo na Shule za Upili za Naitiri na Cardinal Otunga (Mosocho). Ana Shahada za Be.D (Nairobi), M.A (Nairobi) na Ph.D (Indiana, Bloomington). Yeye ni mhadhir mwandamizi katika Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika, Chuo Kikuu cha Kenyatta ambako anafundisha Nadharia za Uhakiki wa Fasihi na Fasihi Leo ya Kiswahili

Reviews
There are no reviews yet.